Nestori

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Nestori wa Konstantinopoli)
Nestori kadiri ya Romeyn de Hooghe (1688)

Nestori (kwa Kigiriki Νεστόριος, Nestorios; Germanicia, (leo nchini Uturuki) 386 hivi – al-Khargah, Misri, 450[1]) alikuwa mmonaki na mwanateolojia aliyefikia kuwa Patriarki wa Konstantinopoli (leo Istanbul) tangu tarehe 10 Aprili 428 hadi Agosti 431, ambapo kaisari Theodosius II alithibitisha uamuzi dhidi yake uliopitishwa na Mtaguso wa Efeso tarehe 22 Juni.

Kwa kukataa jina lililozoeleka la Θεοτόκος, Theotokos, "Mama wa Mungu", kwa Bikira Maria, alisababisha mabishano makubwa na hatimaye mafarakano kuhusu fumbo la Yesu Kristo.

Hasa Sirili wa Aleksandria alimpinga vikali kwa kudai haamini umungu wa Yesu, ingawa mwenyewe alizidi kujitetea hadi kifo chake kwamba anashika imani sahihi.

Anaheshimiwa na Kanisa la Asiria kama mtakatifu. Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 25 Oktoba.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Nestorius Archived 7 Desemba 2017 at the Wayback Machine. Ecumenical Patriarchate

Vyanzo[hariri | hariri chanzo]

  • Meyendorff, John (1989). Imperial unity and Christian divisions: The Church 450-680 A.D. The Church in history. Juz. 2. Crestwood, NY: St. Vladimir's Seminary Press. ISBN 978-0-88-141056-3. {{cite book}}: Invalid |ref=harv (help)
  • Artemi, Eirini,«Τό μυστήριο της Ενανθρωπήσεως στούς δύο διαλόγους «ΠΕΡΙ ΤΗΣ ΕΝΑΝΘΡΩΠΗΣΕΩΣ ΤΟΥ ΜΟΝΟΓΕΝΟΥΣ» και «ΟΤΙ ΕΙΣ Ο ΧΡΙΣΤΟΣ» του Αγίου Κυρίλλου Αλεξανδρείας», in Εκκλησιαστικός Φάρος, ΟΕ (2004), 145–277.
  • St. Cyril of Alexandria: The Christological Controversy ISBN 0-88141-259-7 by John Anthony McGuckin—includes a history of the Council of Ephesus and an analysis of Nestorius' Christology.
  • Edward Walford, translator, The Ecclesiastical History of Evagrius: A History of the Church from AD 431 to AD 594, 1846. Reprinted 2008. Evolution Publishing, ISBN 978-1-889758-88-6. http://www.evolpub.com/CRE/CREseries.html#CRE5 Archived 7 Juni 2015 at the Wayback Machine.—includes an account of the exile and death of Nestorius, along with correspondence purportedly written by Nestorius to Theodosius II.
  • Bishoy Youssef (2011). "Lecture II: The Nature of Our Lord Jesus Christ." http://www.suscopts.org/messages/lectures/christlecture2.pdf
  • Seleznyov, Nikolai N., "Nestorius of Constantinople: Condemnation, Suppression, Veneration, with special reference to the role of his name in East-Syriac Christianity" in: Journal of Eastern Christian Studies 62:3–4 (2010): 165–190.
  • Chesnut, Roberta C. (1978). "The Two Prosopa in Nestorius' Bazaar of Heracleides". The Journal of Theological Studies (29): 392–409. {{cite journal}}: Invalid |ref=harv (help)

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.