Lango:Afrika/Makala iliyochaguliwa
Makala iliyochaguliwa[hariri chanzo]
- 01 Januari 2012 : Nembo ya Uganda
- 01 Februari 2012 : Chuo Kikuu cha Cape Town
- 01 Machi 2012 : Eratosthenes
- 01 Aprili 2012 : Kampeni za Kivita katika Afrika ya Mashariki (Vita ya Kwanza ya Dunia)
- 01 Mei 2012 : Zanj
- 01 Juni 2012 : Jimbo Katoliki la Zanzibar
- 01 Julai 2012 : Assia Djebar
- 01 Agosti 2012 : Hifadhi ya Taifa ya Hell's Gate
- 01 Septemba 2012 : Ziwa Nakuru
- 01 Oktoba 2012 : Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Mashariki
- 01 Novemba 2012 : Hifadhi ya Serengeti
- 01 Desemba 2012 : Chuo Kikuu cha Addis Ababa
Makala iliyochaguliwa kwa Juni 2012[hariri chanzo]
Jimbo Katoliki la Zanzibar (kwa Kilatini Dioecesis Zanzibarensis) ni mojawapo kati ya majimbo 33 ya Kanisa Katoliki nchini Tanzania, likienea katika visiwa vya Unguja na Pemba vya Tanzania visiwani, jumla kilometa mraba 2,332. Makao makuu yake ni katika mji wa Zanzibar na linahusiana na Jimbo kuu la Dar-es-Salaam. Kanisa kuu limewekwa wakfu kwa heshima ya Mtakatifu Yosefu. Askofu wa jimbo ni Augustine Ndeliakyama Shao, C.S.Sp. Jimbo liliundwa rasmi tarehe 28 Machi 1980 baada ya kujitegemea tangu 12 Desemba 1964 kama Apostolic Administration. Hata hivyo historia ni ndefu zaidi, kwa kuwa tangu mwaka 1860 Zanzibar ilikuwa makao makuu ya Apostolic Vicariate. Waumini ni 9.900 kati ya wakazi 990.900 (sawa na 1%), wengi wao wakiwa Waislamu. Mapadri ni 19, ambao kati yao 15 ni wanajimbo na 4 ni watawa. Hivyo kwa wastani kila mmoja anahudumia waumini 521 katika parokia 7. Mabruda jimboni ni 5, na masista 48.