Kanoaldi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kanoaldi (pia: Chagnoald, Cagnoald, Canoeld, Cagnou, Canoaldus; karne ya 6 - 633 hivi) alikuwa askofu wa 6 wa Laon (Ufaransa)[1] baada ya kuwa mmonaki huko Luxeuil chini ya Kolumbani (594)[2] .

Huyo alipofukuzwa na mfalme Theuderiki II (610), Kanoaldi alikwenda naye kuinjilisha eneo la Bregenz, kando ya ziwa la Konstanz (Ujerumani) [3], halafu aliongozana naye hadi Roma.

Hatimaye aliweza kuongoza jimbo lake hadi alipofariki dunia[4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu kama ndugu zake Faro na Fara[5].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Septemba[6].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Abbé Charpentier, Hagiographie laonnoise, Saint Canoeld Cagnoald ou Cagnou 6e evêque de Laon élu en 625 et mort en 638 ou 640, Chauny, 1882.
  • Gilles Cugnier, Histoire du monastère de Luxeuil à travers ses abbés, 590-1790, Langres, imprimeur D. Guéniot, 2003.
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.